Watu Kutaka pesa za haraka na kwa pupa

(Tamaa)

Hili ni tatizo ni kubwa sana miongoni mwa vijana

wengi wa Tanzania na Africa kwa ujumla, utakuta

kijana akishapata uelewa kidogo juu ya bitcoin

anaanza kutafuta sehemu ya kuwekeza kwa haraka

pasipokuwa na uhakika juu ya usalama wa kampuni

hiyo ila anawekeza kwasababu tu ameambiwa

inalipa vizuri na yeye anataka pesa za haraka..

mwisho wa siku anajikuta kampuni hiyo inapotea

mtandaoni na anakula hasara na baadae na yeye

anaanza kuamini kuwa cryptocurrency ni utapeli au

wizi na baadae anakata tamaa juu ya crptocurrency

na kuwathibitishia watu wa jamii inayomzunguka

kuwa cryptocurrency sio salama, kumbe yeye ndio

alikurupuka na kufanya maamuzi yasiyo sahii pia

hakupata uelewa wa kutosha juu ya fursa hii.