Bitcoin ni nini?

Bitcoin ni aina ya sarafu ya kimtandao.

Kama zilivyo pesa nyingine,Ila Bitcoin haina mamlaka yeyote inayoisimamia.

Shughuli za Bitcoin zinawezeshwa kwa maelfu ya computer zilizoenea ulimwengu Mzima, Mtu yeyote anauwezo wa kuwezesha miamala ya bitcoin kwa kudownload aplikesheni maalum.

Historia ya Bitcoin.

Bitcoin ni Sarafu ya kwanza ambayo ilitambulishwa Mwaka 2008, lakini ikaanza kutumika mwaka 2009,

Mfumo huu unamuwezesha mtumiaji yeyote kutuma au kupokea kwa kutumia internet .

Moja ya mambo mambo yanayoifanya Bitcoin kuvutia watu wengi

-Kutokuwa na uwezo kuingiliwa(kuhakiwa) au kuuharibiwa.

-Miamala katika mfumo huu inaweza kufanyika wakati wowote.

-Hauruhusu pesa kutumika zaidi ya mara moja(double spending).

-Pia uhuru wa kufanya miamala kwa maana hakuna mamlaka yoyote inayoucontrol mfumo huu.